- 823 viewsDuration: 2:44Viongozi wa upinzani wameendelea kuikosoa serikali kufuatia kupanda kwa bei ya mafuta nchini. Akiongozwa na Kinara wa Wiper Kalonzo Musyoka, wanasiasa hawa waliokuwa Kaunti ya Kiambu hii leo wamedai kuna njama fiche kutoka kwa serikali kuwanufaisha watu fulani kupitia sekta ya mafuta. Aidha, Kinara wa DCP Rigathi Gachagua, ambaye yuko katika ziara nchini Uingereza, ameendelea kuzungumzia siasa za mafuta katika ziara yake. Willy Lusige na mengi zaidi.