- 119 viewsViongozi wa Kaunti ya Murang’a wanaounga mkono serikali wamesema kuwa eneo hilo linanufaika pakubwa kwa kusimamam na serikali wakipuuza mabadiliko yoyote ya kisiasa. Wakizungumza eneobunge la Kangema, Kaunti ya Murang’a, viongozi hao wakiongozwa na Waziri wa Ardhi na Nyumba, Alice Wahome, wamesema kaunti hiyo inaendelea kufaidi kwa kusimama na serikali ya Kenya Kwanza.