- 199 viewsWaasi wa kikundi cha Hayat Tahrir al-Sham (HTS) wamesema walikuwa wameikamata miji ya Syria ya Talbis na Rastan. Hatua hiyo imewafikisha ndani ya kilometa kadhaa karibu na mji wa Homs, kanda za video katika mitandao ya kijamii Ijumaa (Desemba 6) zinaonyesha kile kilichosemwa ni waasi wakipita na magari katika mji wa Rastan. Kanda ya video hiyo iliyochukuliwa kutoka juu ya jengo moja, iliwaonyesha wapiganaji hao wakipita na magari na pikipiki wakifyatua risasi hewani kusherehekea wakati msafara huo ulipopita mjini humo. Shirika la Habari la Reuters liliweza kuthibitisha eneo hilo kuwa ni Rastan, mji ulioko takriban kilomita 20 kaskazini mwa Homs, kutokana na mpangilio wa mitaa, majengo, mnara wa msikiti na mnara wa saa unaonekana kutoka mbali unaofanana na picha za satalaiti na picha za kumbukumbu. Reuters haikuweza kuthibitisha tarehe maalum video hiyo ilichukuliwa, lakini Kikundi kinachofuatilia haki za binadamu Syria kimeripoti kuwa mji huo ulichukuliwa na waasi Ijumaa (Desemba 6). Mashambulizi ya mabomu yaliyofanywa na Russia usiku kucha yameharibu daraja la Rastan katika barabara kuu ya M5, ambayo ndiyo njia kuu kwenda Homs, kuwazuia waasi hao kulitumia kusonga mbele, afisa wa jeshi wa Syria ameiambia Reuters. Hezbollah imetuma idadi ndogo ya “vikosi vya uangalizi” kutoka Lebanon kwenda Syria usiku kucha kuwasaidia kuzuia waasi wanaipinga serikali kuukamata mji wa kimkakati wa Homs, maafisa wawili wa ngazi ya juu w wa Lebanon wameiambia Reuters. Afisa wa jeshi la Syria na maafisa wawili wa kanda ambao wako karibu na Tehran pia wameiambia Reuters kuwa vikosi maalum kutoka kikundi kinachoungwa mkono na Iran, Hezbollah walivuka kutoka Lebanon na kuingia Syria usiku kucha na wameanza ulinzi wa Homs. - Reuters #waasi #hayattahriralsham #syria #tablis #rastan #hezbollah #iran #voa #voaswahili
Waasi wa Hayat Tahrir al-Sham waiteka miji miwili chini ya serikali
- 6 Aug 2025 - A woman has been found guilty of killing her lover back in 2020 in Nanyuki County.
- 6 Aug 2025 - Human rights activists are calling for the disbandment of the National Police Service (NPS) following damning revelations in the latest EACC corruption index, which ranks the security organ among the most corrupt institutions in the country.
- 6 Aug 2025 - Cabinet Secretary for Public Service Geoffrey Ruku has issued a stern warning to corrupt public officers, calling on the Ethics and Anti-Corruption Commission (EACC) to swiftly arrest all individuals implicated in recent graft reports.
- 6 Aug 2025 - Former Deputy President Rigathi Gachagua has declared his support of the proposal for the United States to review Kenya's designation as a major non-North Atlantic Treaty Organization (NATO) ally.
- 6 Aug 2025 - Six senior officials from the Busia County Government have been arrested over allegations of misappropriating public funds through irregular procurement processes involving tenders worth Ksh.1.4 billion.
- 6 Aug 2025 - In a historic move to combat one of the most common sexually transmitted infections (STIs), the National Health Service (NHS) has launched the world’s first gonorrhoea vaccination programme in England, targeting individuals most at risk of infection.
- 6 Aug 2025 - The government has already threatened to sack police officers and chiefs in some parts of the country.
- 6 Aug 2025 - Ring-necked parrots, green- and yellow-fronted canaries intercepted at Lagos Airport
- 6 Aug 2025 - Nairobi Traffic Commandant Joseph Chirchir said roads near Moi International Sports Complex, Kasarani and Nyayo National Stadium will face full or partial closures to ease movement around the stadium.
- 6 Aug 2025 - Kiambu is among the nine counties that make up the Mount Kenya Bloc.