- 379 viewsWabunge wa UDA kutoka Mlima Kenya sasa wanamtaka katibu mkuu wa chama hicho Hassan Omar kujiuzulu la sivyo watamuandikia kinara wa chama hicho Rais William Ruto kumuondoa ofisini. Wabunge hao wanasema kuwa matamshi ya Hassan Omar wiki iliyopita yamekiuka msimamo wa chama hicho wa kuwaleta Wakenya wote pamoja bila kujali kabila wala dini. Haya yanajiri huku viongozi wa ODM wakikutana na wajumbe wa Kaunti ya Kisumu wakipigia debe muungano wao na Rais Ruto.