- 917 viewsKundi la wabunge wanaomuunga mkono kinara wa DCP Rigathi Gachagua limemkashifu mwenyekiti wa chama cha UDA Cecily Mbarire kufuatia barua aliyomwandikia Rais mstaafu Uhuru Kenyatta, iliyodai kuwa utawala wake kama rais ulichangiwa pakubwa na utendakazi wa serikali ya Kenya Kwanza. Wakizungumza katika eneo la Gikondi, Mukurwe-ini Kaunti ya Nyeri, wabunge hao waliohudhuria hafla ya ufadhili wa masomo wamewaonya wanaomshambulia rais mstaafu mara kwa mara wakisema ana haki ya kujieleza kama Mkenya.