Watu 100 ambao walikuwa wakichimba madini kinyume cha sheria katika mgodi wa dhahabu usiofanya kazi nchini Afrika Kusini walifariki baada ya kunaswa chini ya mgodi huo kwa miezi kadhaa, huku polisi wakijaribu kuwaondoa huko, kundi linalowakilisha wachimba migodi hao lilisema Jumatatu.
Sabelo Mnguni, msemaji wa jamii zilizoathiriwa na uchimbaji madini aliliambia shirika la habari la Associated Press kwamba simu ya mkononi iliyotumwa juu ya mgodi huo na baadhi ya wachimba migodi waliookolewa siku ya Ijumaa, ilikuwa na video mbili zikionyesha miili kadhaa iliyofunikwa kwa plastiki chini ya ardhi.
Mnguni alisema “takriban watu 100 walifariki katika mgodi katika mkoa wa kaskazini magharibi ambako polisi walianzisha operesheni mwezi Novemba kuwalazimisha wachimba migodi kuondoka.
Wanashuku watu hao walikufa kwa njaa au kwa sababu ya kukosa maji mwilini, Mnguni alisema.
Alisema miili 18 iliondolewa ndani ya mgodi huo tangu Ijumaa.
Msemaji wa polisi Brigedia Sebata Mokgwabone alisema bado wanachunguza taarifa kujua ni miili mingapi iliyopatikana na ni manusura wa ngapi waliookolewa baada ya operesheni ya uokoaji kuanzishwa Jumatatu.
-AP
#Stilfontein #madini #mgodi #dhahabu #wachimbaji #afrikakusini #wachimbajiharamu #voa #voaswahili
10 Feb 2025
- The Church of England's elected governing body will begin a week-long meeting on Monday, after an "unprecedented crisis" triggered by a number of sexual abuse scandals.
10 Feb 2025
- President Ruto on Monday maintained that Kenya remains a committed partner in ensuring regional and international peace and security is achieved.
10 Feb 2025
- The Senate is set to resume its sittings on Tuesday at 2:30 PM, marking the beginning of the Fourth Session of the 4th Senate. This session follows a long recess that began in early December 2024 and is expected to address key legislative and financial…
10 Feb 2025
- Police officers in Ruai, Nairobi County are probing an incident where rogue police officers raided a woman’s house in demand of Ksh.20 million allegedly stolen from a Kenyan Senator
10 Feb 2025
- Kenya, Uganda and Nigeria are the only countries in Africa that have enacted climate change legislations, according to study by African Group of Negotiators, Expert Support (AGNES).