- 1,675 viewsDuration: 2:14Wafanyabiashara katika Soko la Ringa, Kaunti ya Homa Bay, sasa wanaitaka idara ya kilimo ya kaunti hiyo kutatua tatizo la nyuki ambao wamekuwa wakiwahangaisha kwa miezi kadhaa. Nyuki hao wamejenga makazi kwenye vigingi vya umeme sokoni humo na huwavamia wateja mara kwa mara. Na kama anavyoarifu Laura Otieno, wafanyabiashara hao wanadai kuwa watu wawili wamefariki baada ya kushambuliwa na nyuki, huku wengine wakiuguza majeraha.