- 7,928 viewsDuration: 1:48Muungano wa wahadhiri nchini uasu umesisitiza kuwa mgomo wa wahadhiri na wafanyikazi wa vyuo vikuu vya umma unaendelea licha ya serkali kukubali kuwa itawalipa shilingi bilioni 7.9 kama malimbikizi ya nyongezo ya mishahara ya 2017-2021. UASU imesema wahadhiri wamekataa kulipwa fedha hizo kwa awamu tatu na wanataka zilipwe zote kwa pamoja. Wahadhiri hao wamepuuza madai ya serikali kuwa masomo yanaendelea katika baadhi ya vyuo vya umma.