- 214 viewsWaislamu kote nchini leo wameungana na wenzao duniani kuadhimisha sherehe za sikukuu ya Eid Ul Adha. Kupanda kwa gharama ya maisha na cheche za siasa zilisheheni jumbe za Eid katika sehemu nyingi. Aidha, Wakenya waliozungumza wameitaka serikali kushusha gharama ya maisha na kuhimiza mshikamano wa kitaifa.