Idara ya madini itafanya mazungumzo na wakazi wa eneo la Ikolomani kaunti ya Kakamega, ili kulainisha mtafaruku kuhusu kibali cha uchimbaji wa dhahabu katika eneo hilo. Akizungumza baada ya mkutano na viogozi kutoka kaunti hiyo, katibu katika idara ua madini, Harry Kimtai, alisema kuwa hakuna leseni itakayotolewa kabla ya jamii kushirikishwa vilivyo. Mkutano huo ulifanyika miezi miwili baada ya watu watatu kuuwawa na wengine sitini kukamatwa baada ya kikao cha kujadili uchimbaji dhahabu kutibuka.