- 994 viewsDuration: 3:30Wakazi wa kaunti za Kilifi na wajir zilizoko miongoni mwa kaunti 23 zinazokabiliwa na baa la njaa wamepokea chakula cha msaada kutoka kwa serikali. Huko malindi, zaidi ya wakazi 3,000 walijitokeza kupokea chakula cha msaada wengi wakilalamika kuwa hakitoshi na kutaka serikali kuanzisha miradi ya kilimo ili kuwakinga na makali ya njaa. Zaidi ya wakenya milioni 3.3 wanakabiliwa na njaa huku serikali ikitoa shilingi bilioni 4.1 kukabiliana na hali hii.