Familia mbili zitakesha tena usiku mwingine mgumu kwenye eneo ambapo jengo liliporomoka mtaani South C Nairobi, huku makundi ya uokoaji yakifanya kila juhudi kujaribu kuwaokoa walinzi wawili wanaoaminika kuwa wamekwama katika vifusi vya jengo hilo. Viongozi kutoka kaunti ya Marsabit wametoa wito kwa serikali iharakishe shughuli za uokoaji. Huku haya yakijiri, uchunguzi wa kisayansi umeanzishwa ili kubaini hasa kilichosababisha ajali hiyo. Joseph Wakhungu ana habari kwa kina.
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc
Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#kbcchannel1 #news #kbclive