- 230 viewsDuration: 3:21Watoto zaidi wa Gredi ya 10 wameendelea kujitokeza kusimulia changamoto wanazokumbana nazo baada ya masomo yao kukwama kutokana na ukosefu wa karo. Mercy Kagendo kutoka eneo la Mishomoroni, Mombasa, bado hajajiunga rasmi na masomo ya Gredi ya 10 licha ya kuwa alishika nafasi ya kwanza katika Shule ya Mtopanga kwa alama 62. Hali hii inajiri wakati Wizara ya Elimu ikijitetea kwamba asilimia 99.5 ya wanafunzi wameripotiwa kuwa shuleni.