- 886 viewsDuration: 2:46Balozi mteule wa Kenya nchini Canada na aliyekuwa Kamishna Mkuu wa KRA, Humphrey Wattanga, amejipata katika njia panda baada ya kushindwa kujibu kikamilifu maswali ya Kamati ya Ulinzi na Mahusiano ya Kigeni iliyomhoji kuhusu uwezo wake. Wattanga alipata wakati mgumu kujibu maswali kuhusu utendaji wake wa awali, tuhuma za uongozi mbovu na kuondoka kwake KRA, huku baadhi ya wajumbe wakieleza wasiwasi kuwa uteuzi wake huenda ukadunisha uhusiano kati ya Kenya na Canada. Willy Lusige anaripoti zaidi.