- 2,807 viewsDuration: 3:26Idadi ya watu walioaga dunia kufuatia maporomoko ya ardhi huko Chesongoch, bonde la Kerio katika kaunti ya Elgeyo-Marakwet imefikia 15 baada ya mili mitano zaidi kupatikana. Waziri wa usalama wa taifa Kipchumba Murkomen alisema kuwa watu 30 bado hawajulikani waliko huku shughuli za uokoaji zikiendelea. Maporomoko hayo yalitokea Jumamosi asubuhi kufuatia mvua kubwa na kusomba nyumba kadhaa. Watu kadhaa wamenusuriwa kwneye operesheni ya pamoja ya jeshi, polisi na shirika la msalaba mwekundu na wanapokea matibabu katika hospitali ya mafunzo na matibabu maalum ya Moi na vituo vingine vya afya. Connect with KBC Online; Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1 Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV Check our website: https://www.kbc.co.ke/ #kbcchannel1 #news #kbclive