- 379 viewsShirika la Afya duniani (WHO) likishirikina na Kituo cha Kudhibiti magonjwa barani Afrika limezindua mpango wa pamoja wa bara afrika wa kupambana na ugonjwa wa Ebola unaosababishwa na virusi vya Bundibugyo. Mpango huo wa kati ya mwezi juni na novemba 2026 unalenga kuchangisha dola milioni 518 kusaidia mataifa ya bara afrika kugundua na kudhibiti ugonjwa huo. W.H.O imeonya mataifa dhidi ya kuweka marufuku ya usafiri na kufunga mipaka ikisema kuwa huenda ikalazimu watu kutumia mipenyo haramu inayoweza kuzidisha kusambaa kwa ugonjwa huo