- 3,976 viewsDuration: 1:59Wanawake zaidi ya laki moja katika eneo la Nyanza hutegemea biashara ya samaki ili kujikimu kimaisha, huku wengi wao wakilazimika kujiingiza katika biashara ya ngono ili kupata samaki ziwani victoria, maarufu kama jaboya. Katika ufuo wa Luanda Kotieno, kaunti ndogo ya Rarieda, Shirika la Shining Hope for Communities (SHOFCO) limeanzisha mpango bunifu wa mashindano ya kuendesha boti, unaolenga kuwapa wanawake fursa mbadala na kurejesha heshima yao.