1,098 views
Duration: 6:08
Kutokana na imani potofu za "meno dhaniwa ya plastiki," "kimeo," ama "udata," watoto wadogo wanafanyiwa ukatili huu wa kinywa, unaofahamika kitaalamu kama Infant Oral Mutilation (IOM).
Ukatili huu umewasababishia watoto maumivu makali, magonjwa na hata vifo, huku ukifanywa na waganga wa kienyeji kwa kutumia vifaa duni visivyo salama.
Kwa mujibu wa Jarida la British Dental Journal, watoto milioni 25 wameathiriwa na ukatili huu Afrika Mashariki ikiwemo Tanzania.
Mwandishi wa BBC Yusuph Mazimu anatuangazia kwa undani ukubwa wa tatizo hili, na jinsi linavyoathiri watoto.
#bbcswahili #tanzania #afya
Subscribe kupata video motomoto kila siku kutoka BBC Idhaa ya Kiswahili https://www.youtube.com/channel/UCoerKKIKIMlDYaVFSTlsWGw