Chama cha KUPPET tawi la Mombasa kimetaja uhaba wa walimu wa masomo maalum katika shule kama changamoto kuu katika sekta ya elimu hasa utekelezaji wa mtaala wa cbe katika gredi ya 10.
Wakiongozwa na katibu wa chama hicho Lynette Kamadi pamoja na baadhi ya walimu wa shule za sekondari, wanadai hadi sasa kaunti za pwani hakuna walimu wa somo la masuala ya anga, ubaharia na masomo ya ufundi. Muungano huo unalalama kuwa shule nyingi kaunti ya mombasa bado zinakumbwa na changamoto ya masomo ya sekondari ya juu.