- 964 viewsDuration: 3:05Asasi za serikali zinazohusika na usalama na maandalizi ya uchaguzi mkuu wa mwaka ujao zimeonya viongozi wenye ndimi za uchochezi dhidi ya kuwarejesha Wakenya kwenye machafuko ya baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2007. Wakizungumza kwenye mkutano wa kujadili hali ya usalama nchini, viongozi hao wakiongozwa na Mwenyekiti wa IEBC, Erastus Ethekon, wameapa kukabiliana na wafadhili wa wahuni wanaovuruga amani kwenye mikutano ya kisiasa.