- 11,978 viewsDuration: 2:39Kinara wa DCP Rigathi Gachagua ameitisha maandamano dhidi ya kuongezwa kwa bei ya mafuta tarehe 25 mwezi Juni sambamba na maandamano ya kuadhimisha dhuluma dhidi ya vijana wa Gen Z. Akihutubia wanahabari kabla ya kuabiri ndege kuelekea nchini Uingereza Ijumaa usiku, naibu rais huyo wa zamani alisema kwamba kuongezeka kwa bei ya mafuta kunatokana na ufisadi, na wala si vita dhidi ya Iran, Israel na Marekani.