- 11,121 viewsDuration: 3:17Waziri wa Biashara Lee Kinyanjui amelaani mashambulizi ya aina yoyote dhidi ya raia wa kigeni nchini na kuwaonya Wakenya dhidi ya kuchukua sheria mikononi mwao. Kinyanjui amesema agizo la Rais William Ruto linalowataka raia wa kigeni wanaoendesha biashara ndogo ndogo kusitisha shughuli zao halipaswi kutumiwa kama sababu ya kuwanyanyasa au kuwashambulia wafanyabiashara hao. Agizo hilo limezua hofu kufuatia ripoti za unyanyasaji na mashambulizi dhidi ya baadhi ya wafanyabiashara wa kigeni. Serfine Achieng Ouma ana kina cha taarifa hii.