- 25,253 viewsDuration: 3:00Rais William Ruto amemshambulia mtangulizi wake, Rais Mstaafu Uhuru Kenyatta, akisema amejiaibisha kwa kung’ang’ania uongozi wa chama cha Jubilee. Akirejelea uamuzi wa mahakama wa Jumatatu uliomzuia Uhuru kuendelea kuwa kinara wa Jubilee, Ruto amesema rais huyo mstaafu ameshusha hadhi ya kiti cha urais. Kama anavyoarifu Emmanuel Too, Ruto aliendelea kujipigia debe katika ziara yake ya Kaunti ya Siaya, akisema serikali jumuishi imekuwa ikitekeleza miradi ya maendeleo bila ubaguzi.