- 3,151 viewsDuration: 1:04Mama aliyelazimika kumwacha mwanawe wa miaka miwili nchini Saudi Arabia amepata fursa ya kuungana naye tena miaka miwili baadaye. Peninah Wanjiru Kinyanjui ameungana na bintiye leo baada ya kutengana alipofurushwa Saudi Arabia kwa kukiuka sheria za uhamiaji. Mtoto Precious Wambui hakuwa na cheti cha kuzaliwa wala nyaraka nyingine za utambulisho wakati huo. Ililazimu Serikali ya Kenya kuingilia kati kuhakikisha Peninah anampata mwanawe salama.