- 1,506 viewsDuration: 2:03Mshukiwa mkuu wa kutekwa nyara kwa watoto wawili wenye umri wa miaka 16 na 17 huko Kiembeni, Kaunti ya Mombasa, amefikishwa kizimbani. Mwanaharakati Caleb Ngwena anadaiwa kuwasafirisha watoto hao hadi Kaunti ya Kiambu, ambako inadaiwa walifungiwa katika nyumba na kudhulumiwa kingono. Mahakama imekubali ombi la upande wa mashtaka la kuwazuilia washukiwa kwa siku 14 ili kukamilisha uchunguzi. Francis Mtalaki ana taarifa zaidi.