- 4,567 viewsDuration: 3:13Wakazi wa eneo la Isinya, kaunti ya kajiado wanalalamikia utovu wa usalama baada ya mwili wa mtoto wa miaka saba aliyeripotiwa kutoweka mapema wiki hii kupatikana umetupwa barabarani. Inaarifiwa kuwa wazazi wa mtoto huyo walipokea simu hapo jana kuwataka walipe pesa za ukombozi kabla ya gunia lililokuwa na mwili wa mtoto huyo kupatikana barabarani hii leo. Na kama anavyoarifu Robert Masai, polisi wanasema wameanzisha uchunguzi kuhusiana na tukio hilo.