- 6,126 viewsDuration: 1:13Mume wa Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, Hafidh Ameir Hassan, anatarajiwa kuzikwa leo katika eneo la Kizimkazi, Zanzibar, saa chache baada ya kuaga dunia alipokuwa akipokea matibabu. Viongozi mbalimbali kutoka Afrika Mashariki wametuma risala za rambirambi kwa Rais Samia kufuatia kifo cha mumewe. Tangazo la kifo cha Hafidh Ameir Hassan lilitolewa na Makamu wa Rais wa Tanzania Deogratius Ndejembi, aliyesema Ameir aliaga dunia mwendo wa saa mbili asubuhi katika Hospitali ya Emilio Mzena Memorial huko Zanzibar, ambako alikuwa akipokea matibabu ya matatizo ya moyo.