Wanasiasa walio na tabia ya kupayuka hadharani na kutoa cheche za maneno sasa wameonywa kuwa watakamatwa. Tume ya Kitaifa ya Uwiano na Utangamano wa Kitaifa NCIC, kwa ushirikiano na viongozi wa kidini wametangaza mikakati ya wanasiasa kuwajibikia matamshi yao. Kwenye kongamano la mashauriano lililofanyika jijini Nairobi, makubaliano yaliafikiwa kuhusu hatua kadhaa, ikiwemo kuzinduliwa kwa kampeni ya kukabiliana na maneno ya chuki, chini ya mwaka mmoja kabla ya Uchaguzi Mkuu, kama anavyoarifu Ben Kirui.