- 6,204 viewsDuration: 2:46Kinara wa Chama cha Peoples Party Ndindi Nyoro amekashifu matamshi ya baadhi ya viongozi kuwatishia wapiga kura kuhama iwapo hawataipigia kura serikali ya Rais William Ruto mwaka ujao. Nyoro amesema kwamba wakenya wote wana haki ya kikatiba kujihusisha na mrengo wowote wa kisiasa. Naye, Naibu kinara wa chama cha Jubilee Fred Matiangi amewashutumu polisi kwa kile anasema ni kutumika na wanasiasa huku Viongozi wa DCP wakisema misimamo yao haitayumba licha ya kukandamizwa na serikali.