- 6 viewsDuration: 2:40Viongozi wa eneo bunge la Rabai, Kaunti ya Kilifi, wamezindua mpango wa hamasa ya nyumba kwa nyumba ili kuwahimiza wananchi kujiandikisha kama wapiga kura kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2027. Hatua hiyo imechukuliwa baada ya takwimu kutoka Idara ya Usajili wa Vitambulisho na IEBC kuonyesha kuwa zaidi ya wananchi 26,000 waliopata vitambulisho vya taifa katika eneo hilo bado hawajajisajili kama wapiga kura.