- 887 viewsDuration: 1:27Rais William Ruto amesisitiza ushirikiano kati ya serikali za kaunti na serikali kuu katika kutekeleza miradi ya maendeleo na kuboresha maisha ya Wakenya. Rais amesema ni sharti kila serikali ielewe na kutekeleza wajibu wake wa kikatiba. Ameyasema hayo Ikulu ya Nairobi alipokutana na magavana na kuongoza hafla ya kuwaapisha wanachama saba wa kamati ya kiufundi kuhusu uhusiano kati ya serikali za kaunti na serikali kuu.