- 34,841 viewsDuration: 3:12Rais William Ruto ametangaza kufungwa kwa Kampuni ya madini ya TATA iliyoko eneo la Magadi, akidai kwamba Kampuni hiyo imefeli kutekeleza wajibu wake kwa wakaazi wa eneo hilo. Rais alitangaza haya kwenye siku ya kwanza ya ziara yake kaunti ya Kajiado. Kwenye taarifa, kampuni hiyo ya Tata imesema kuwa ilifuata maagizo yote yaliyotolewa na serikali ila juhudi zao ziligonga mwamba.