- 5,143 viewsDuration: 2:44Rais William Ruto amesisitiza kuwa serikali yake imeweka kila juhudi kutekeleza mapendekezo ya kuleta mageuzi katika idara za usalama nchini, akipuuza madai yanayotolewa na wapinzani wake. Akizungumza katika mahafali ya Polisi wa Utawala huko Embakasi, Ruto amesema serikali yake haipingi kuchunguzwa kuhusu utekelezaji wa majukumu yake. Hata hivyo, amewataka wapinzani kukosoa serikali kwa ukweli na ushahidi.