- 4,603 viewsDuration: 3:27Viongozi wa ukanda wa magharibi wamemsuta kinara wa chama cha DAP-K Eugene Wamalwa kwa kile wanachotaja kuwa jaribio la kuugawanya ukanda wa magharibi, kabla ya uchaguzi ujao. Wamalwa aliyezomewa kwa kushabikia umoja wa waluhya kwa upande mmoja na kuvuta kwingine na chama chake, ameshauriwa kuvunja DAP-K na kushirikiana na wenzake, kumuunga mkono rais William ruto mwaka 2027 kwa Muhula wa pili. Naye rais mstaafu Uhuru Kenyatta ameendelea kushambuliwa na wandani wa Rais, akishtumiwa kwa kuchangia mpasuko ndani ya ODM.