- 8,257 viewsDuration: 2:18Wabunge wa kike wameshutumu vikali matamshi ya aliyekuwa naibu Rais Rigathi Gachagua kuwa mke wa waziri usalama kipchumba murkomen arudishwe eneo la mlimani mlima kenya kwa kuwa ni mtoto wao. Wamekashifu matamshi hayo wakisema ni ya ukabila na wanawake hawachagui mahali wanapokwenda kuolewa wala kabila. Wamewahimiza wakenya kupuuzilia mbali siasa ya kugawanya wakenya kwa msingi wa kijinsia na ukabila. Walikuwa wakiongea katika majengo ya bunge hapa jijini nairobi.