Wakazi wa Mtepeni, Kaunti ya Kilifi, leo wameanzisha mradi wa ujenzi wa bomba la maji safi wakisema mkandarasi amefunga barabara ya kuingia katika nyumba zao.
Wakazi hao waliojaa ghadhabu walifanya maandamano wakilalamika kuwa kwa siku tatu wamekosa mahali pa kupita na wanafunzi watakosa masomo endapo suluhu haitapatikana. Baadhi ya wakazi wamelazimika kutoa magari yaliyokwama huku wakionya mtaro wa bomba la maji ni hatari kwa usalama wa watoto. Maafisa wa shirika la kusambaza maji Kaunti ya Kilifi, KIMAWASCO, walizuru eneo hilo wakiahidi kutatua mzozo huo.