- 1,186 viewsDuration: 2:56Wakazi wa nyumba za New Mukuru, zilizojengwa chini ya mradi wa serikali wa boma yangu, sasa wanalalamikia kucheleweshwa kwa fedha za kuwasaidia kuhama, miezi sita baada ya kuhamia nyumba zao mpya. Kila nyumba ilitarajiwa kupokea shilingi 30,000 kuwasaidia kujipanga upya. Hata hivyo, wakazi wengi wanasema fedha hizo bado hazijatolewa, hali inayozua hofu kuwa huenda wakanyimwa haki yao.