- 5,643 viewsDuration: 2:50Watu wawili wameuawa katika mapigano mapya katika mpaka wa Transmara na Kisii. Watu wengine kadhaa wamejeruhiwa huku mashamba kadhaa yakiteketezwa kufuatia mapigano hayo. Maafisa wa usalama kutoka Kisii na Narok wamefanya mkutano wa dharura katika eneo la mpakani kutathmini hali, huku usalama ukiendelea kuwa tete. Na kama anavyoripoti Chrispine Otieno, wenyeji wameelezea wasiwasi wao, wakisema shughuli za usafiri pamoja na huduma muhimu zimetatizwa kutokana na hali hiyo.