- 1,499 viewsDuration: 3:32Wauguzi nchini wamesitisha mgomo wao ulioendelea kwa siku 43, baada ya kuafikia makubaliano ya kurejea kazini na Baraza la Magavana. Magavana, ambao awali walitaja matakwa ya wauguzi hao kuwa mazito kutekelezwa sasa wameafiki kushughulikia maswala muhimu kama vile marupurupu ya sare na kuajiriwa kwa wauguzi wa UHC. Hata hivyo kama Mary Muoki anavyoarifu, imekuwa siku nyingine ya mahangaiko ya wagonjwa waliofika hospitali za umma kutafuta huduma za matibabu