- 147 viewsDuration: 1:42Shule zaidi ya 10 za msingi katika Kaunti Ndogo ya Nyatike zimezindua programu ya kupanda miti inayolenga kukuza hulka ya uhifadhi wa mazingira na kupunguza athari za mabadiliko ya tabia nchi katika eneo hilo. Mpango huo, unatekelezwa chini ya programu ya “Adopt a Tree” ambapo kila mwanafunzi anatarajiwa kupanda na kutunza mti hadi ukomae. Walimu waliohusika katika awamu ya majaribio wanasema programu hiyo itasaidia wanafunzi kuelewa umuhimu wa uhifadhi wa mazingira wakiwa wadogo..