- 2,372 viewsDuration: 2:37Kikosi cha Ulinzi cha Kenya kimekamilisha usajili wa makurutu kote nchini hivyo kuashiria mwisho wa awamu ya kwanza ya shughuli hiyo mwaka huu. Makamu mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Luteni Jenerali John Omenda akizuru kituo cha usajili cha Kikuyu katika Kaunti ya Kiambu, alisema shughuli hiyo iliendelea vyema. Kikosi cha ulinzi cha Kenya sasa kinatarajiwa kuelekea katika awamu inayofuata ya kusajili wafanyikazi na wanawake mapema mwezi ujao, huku makurutu waliofuzu kutokana na shughuli iliyokamilika, wakijiandaa kuanza mafunzo huko Eldoret. Ben Chumba ana taarifa kamili. Connect with KBC Online; Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1 Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV Check our website: https://www.kbc.co.ke/ #kbcchannel1 #news #kbclive