- 1,171 viewsAliyekuwa mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka ya Kenya (IEBC), Wafula Wanyonyi Chebukati, aliaga dunia jana Alhamisi katika hospitali moja mjini Nairobi akiwa na umri wa miaka 63, baada ya kuugua kwa muda mrefu, kama ilivyothibitishwa na familia yake. Chebukati aliteuliwa kuwa mwenyekiti wa IEBC mwaka 2017 na Rais wa wakati huo Uhuru Kenyatta. Kipindi chake kama mwenyekiti wa tume hiyo kilikumbwa na changamoto nyingi zikiwemo za kusimamia chaguzi za mwaka 2017 na 2022 zilizoghubikwa na utata. Matokeo ya uchaguzi wa urais wa 2017 yalibatilishwa na Mahakama ya Juu kwa sababu ya kasoro, na kusababisha uchaguzi wa marudio. Katika uchaguzi wa 2022, Chebukati alimtangaza William Ruto kama Rais mteule, akimshinda mpinzani wake wa karibu, Raila Odinga, huku kukiwa na mgawanyiko ndani ya tume hiyo. Makamishna wanne walipinga matokeo hayo na kusababisha mtafaruku mkubwa wa kisisa katika taifa hilio la Afrika Mashariki. Licha ya mzozo wa ndani na shinikizo kutoka nje, Chebukati aliendelea kutetea matokeo yaliyotangazwa, ambayo baadaye yaliidhinishwa na Mahakama ya Juu. Kipindi chake pia kilikumbwa na matukio ya kusikitisha, ikiwa ni pamoja na vifo vya maafisa wa IEBC Chris Msando 2017 na Daniel Musyoka 2022. Rais William Ruto aliomboleza kifo cha Chebukati akimtaja kuwa kiongozi aliyetumikia taifa kwa uadilifu, akisema kuwa kifo chake ni hasara kubwa kwa taifa. Chebukati ameacha mjane Mary Chebukati Wanyonyi, ambaye aliteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Ugavi wa Mapato 2023, na watoto kadhaa. - VOA Swahili #IEBC #WafulaWanyonyiChebukati #kifo #maombolezi #Rais #kenya #williamruto
Mwenyekiti wa zamani wa IEBC afariki akiwa na umri wa miaka 63
- 16 Jun 2025 - Former Deputy President Rigathi Gachagua has urged the Kenyan youth to avoid taking to the streets on June 25 to commemorate the deadly aftermath of the anti-tax protests , warning that there is a plot to kill them.
- 16 Jun 2025 - Former Chief Justice David Maraga now wants president William Ruto to take action following the heinous murder of teacher Albert Ojwang', saying the buck stops with him as the head of government.
- 16 Jun 2025 - The Independent Policing Oversight Authority (IPOA) has filed a miscellaneous application seeking to detain Nairobi Central Police Station OCS, Samson Taalam, for 21 days to allow completion of investigations into the gruesome murder of blogger Albert…
- 16 Jun 2025 - The medics allege a sinister plot by the government.
- 16 Jun 2025 - This is the latest government plan slated to benefit ordinary Kenyans.
- 16 Jun 2025 - Treasury Cabinet Secretary John Mbadi has reiterated that the 2025/2026 Budget is specifically tailored for the ordinary Kenyan, taking into account fiscal responsibility, tax relief, and enhanced efficiency in public spending. Addressing concerns…
- 16 Jun 2025 - Ojwang, a blogger and teacher, died on June 7 while in custody at Central Police Station.
- 16 Jun 2025 - The CVR captures audio from the cockpit, including pilot conversations, alarms and ambient sounds.
- 16 Jun 2025 - The People’s Liberation Party leader Martha Karua has slammed President William Ruto over his recent remarks suggesting he would not hand over power if he loses the 2027 general election, saying the Constitution is clear that transfer of power is a…
- 16 Jun 2025 - The directors argued that they were employees and had been unfairly dismissed; the party argued that they were not employees but consultants.