Baraza la wazee wa jamii ya Kikuyu limepinga pendekezo la kurekebisha Katiba kupitia kura ya maamuzi itakayofanyika kwa wakati mmoja na uchaguzi mkuu wa mwaka 2027. Hatua hii inajiri siku moja tu baada ya waziri mwenye mamlaka makuu, Musalia Mudavadi, kusema kuwa huu ndio wakati mwafaka wa kurekebisha katiba alipohudhuria hafla ya kitamaduni katika kaunti ya Vihiga. Viongozi wa upinzani, akiwemo kiongozi wa chama cha DAP-K, Eugene Wamalwa, pia wamepuuzilia mbali wito huo wakisema kuwa sio swala muhimu kwa Wakenya kwa sasa.
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc
Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#kbcchannel1 #news #kbclive