- 1,430 viewsDuration: 3:58Wasiwasi umeanza kuwakumba wasimamizi wa shule za sekondari za kutwa za juu nchini kutokana na idadi ndogo ya wanafunzi waliofika shuleni kufikia sasa. Katika baadhi ya shule, ni chini ya wanafunzi kumi waliofika, licha ya zaidi ya 100 kutarajiwa. Haya yanajiri huku baadhi ya wanafunzi wa gredi ya 10 waliopita wakisalia nyumbani licha ya serikali kuagiza kampeni kuwatafuta wanafunzi hao.