- 460 viewsDuration: 2:16Huku maeneo mbali mbali yakiendelea kukabiliwa na baa la njaa kutokana na makali ya kiangazi serikali imetakiwa kuwekeza zaidi katika ukulima endelevu hasa mashinani. Wakizungumza katika uzinduzi wa mradi wa ukulima endelevu uliofadhiliwa na shirika moja lisilokuwa la kiserikali la Gapeka Children Hope Center katika eneo la Langobaya kaunti ya Kilifi, wadau wa kilimo katika eneo hilo wamesema kutokana na mabadiliko ya tabia nchi ipo haja kwa serikali kuwezesha wakulima wadogo wadogo kupitia ukulima wa kisasa kama njia moja ya kupunguza makali ya kiangazi.