- 7,099 viewsDuration: 2:48Viongozi wa Upinzani wameahidi kumuondoa mamlakani Rais William Ruto kwenye kinyang’anyiro cha urais mwaka ujao. Wakizungumza eneo la Njabini kaunti ya Nyandarua, vinara hao Rigathi Gachagua wa DCP, Fred Matiang’I wa Jubilee na Justin Muturi wa DP, wanasema wanajipanga na sera mbadala wanazoandaa kufanikisha uongozi bora kwa taifa. Aidha wamewarai vijana kujisajili kwa wingi kama wapiga kura na kuusaidia upinzani kumbandua Rais Ruto Mamlakani.