Shirika la Utangazaji nchini lilianza wiki ya Redio Duniani kwa mfululizo wa shughuli mbalimbali kabla ya Siku ya Redio Duniani iliyopangwa kuadhimishwa Ijumaa hii. Miongoni mwa shughuli hizo ni maonyesho yanayofuatilia mabadiliko ya redio kutoka enzi ya analogi hadi mawimbi ya kidijitali. Mada kuu ya kimataifa ya Siku ya Redio Duniani ya mwaka huu ni "Redio na akili mnemba; uvumbuzi unaowezesha, maadili yanayohamasisha, uaminifu unaodumu". Inaangazia jinsi akili mnemba au AI inavyoweza kuimarisha jukumu la redio bila kuchukua nafasi ya sauti ya binadamu. Mwandishi wetu John Kairo ana maelezo.
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc
Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#kbcchannel1 #news #kbclive