Ziara ya rais William Ruto kaskazini mwa nchi imevutia hisia mbalimbali kutoka kwa wakazi ambao wameelezea matarajio yao.
Katika kaunti ya Garissa, wakazi wanaitaka serikali kuongeza miradi ya maendeleo, kando na kufungua mpaka wa Kenya na Somalia ili kuimarisha viwango vya biashara kati ya mataifa hayo.Viongozi hao wamesema serikali inapoteza mapato mengi kupitia biashara za magendo, ambazo pia zinachangia visa vya uhalifu eneo hilo.Viongozi hao pia wanaitaka serikali kujenga barabara kutoka Garissa mjini hadi Liboi ili kupunguza mashambulizi ya mabomu za kutegwa ardhini.