- 467 viewsDuration: 3:32Baraza la magavana sasa limetishia kuwasilisha majina ya maseneta wanaoitisha hongo katika vikao vya kamati ya seneti ya uhasibu na kuhujumu utendakazi wa magavana. Mwenyekiti wa baraza la magavana Ahmed Abdullahi amemuandikia barua spika wa seneti Amason Kingi kuandaa kikao cha dharura na magavana la sivyo hawatafika mbele ya seneti kujibu maswali.