Idara ya utabiri wa hali ya anga imewahimiza wakazi kwenye maeneo kame nchini kutumia ushauri unaotolewa na idara hiyo vilivyo ili kuepuka hasara ya mali na maaafa .
Akizungumza huko Masalani kaunti ya Garissa, kaimu mkurugenzi wa idara hiyo, Edward Muriuki, amesema ushauri huo utawezesha serikali ya kaunti hiyo kuweka mipango maalum ya kukabiliana na majanga. Aidha wafugaji wanashauriwa kuuza baadhi ya mifugo wao na kujiandaa kununua wengine msimu wa mvua. Kulingana na utabiri huo, mvua katika eneo la Kaskazini Mashariki zinatarajiwa kuwa za kiwango cha wastani, kuashiria hali ya ukame itaendelea kwa muda.